Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baada ya matukio ya mauaji, mengine yaibuka Mbeya

Jumatatu , 18th Feb , 2019

Baadhi ya wananchi wanaoishi katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, wameingiwa na hofu baada ya kuibuka wimbi la ubakaji wa watoto unaotekelezwa na watu wasiojulikana huku vitendo hivyo vikihusishwa na imani za kishirikina.

Picha hii haihusiani na habari

Mpaka sasa watoto wanne wamenusurika kubakwa huku wabakaji hao wakifanikiwa kumbaka mtoto mmoja ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Mapinduzi alipokuwa akitoka akitoka shuleni jioni.

Diwani wa eneo hilo, Kasmine Mwangomale amewataka watumishi wa kiroho wakiwemo wachungaji kukiweka kitongoji hicho mikononi mwa Mungu ili matukio kama hayo yaweze kukoma, huku akieleza kuwa mara nyingi maiti zinaokotwa zikiwa zimetelekezwa sehemu mbalimbali kwa muda mrefu.

Naye Mchungaji wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Vumilia Mwasenga, ameeleza kuwa Februali 17 mwaka huu walipokuwa kanisani wanaendelea na ibada, mtu mmoja alitaka kuwabaka watoto watatu wenye kati ya miaka 12 na 13.

Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Mbeya, Debora Hokololo, amesema Jeshi la Polisi litafanya kila namna kuhakikisha wahusika wa matukio hayo wanakamatwa na kushughulikiwa na kuwataka wazazi na walezi kuimarisha ulinzi wa watoto wao kwa kuhakikisha hawawaachi peke yao majumbani ama kuwatuma peke yao kwenda madukani nyakati za usiku.

"Ina maana mnataka tuwalinde watoto wetu kama yanayotokea kule Njombe?, kule wameua na sisi tunaanza kubaka. Haya ni matunda ya kuwasikiliza waganga, naagiza kesi zote za matukio haya zifunguliwe", amesema OCD wa wilaya ya Mbeya, Debora Hokololo.
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA