Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baba amtelekeza mke kisa mtoto kuugua 

Jumatatu , 12th Apr , 2021

Imani potofu kwenye baadhi ya magonjwa ambayo yanawakabili watoto imepelekea kuvunja ndoa ya Zawadi Juma (18) baada ya kuzaa mtoto mwenye tatizo la ubongo maji, ambalo limekuwa likimsumbua tangu kuzaliwa kwake na kupelekea baba wa mtoto kumfukuza nyumbani.

Pichani Zawadi Juma akiwa na mwanae.

EATV ilifika nyumbani kwa mjomba wake na Zawadi ambapo tangu afukuzwe na mume wake ndipo mahali anapoishi naye anaelezea ugonjwa huo ulivyomuanza mtoto wake. 

"Nilijifungulia kwenye kituo cha afya Katoro tukaenda nyumbani, mtoto akamaliza wiki mbili akaanza kuugua kama vile degedege, tulilazwa hospitali akachomwa sindano tukaambiwa twende nyumbani na tuliambiwa tukiona mtoto kichwa kimeanza kukua tuwahi kumrudisha," amesema Zawadi Juma mama wa mtoto huyo.

Amesema alipoona mtoto kichwa kinaanza kukua alimwambia mumewe maelezo waliyopewa hospitalini amabapo mumewe alimjibu kuwa mtoto anakua hivyo amuache ijapokuwa kukua kwa kichwa cha mtoto huyo sio kwa kawaida.

Aidha, zawadi amewaomba Watanzania walioguswa na tatizo la mwanae waweze kumsaidia mtoto wake apone ili na yeye aweze kufanya shughuli za kumuingizia kipato, kwani mumewe amemfukuza nyumbani mpaka mtoto atakapofariki dunia ndipo warudiane.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa mkoa wa Geita, Dkt. Japhet Simeo, anasema tatizo hilo linaweza likampata mtu wa umri wowote na matibabu yanapatikana hivyo amewaomba wananchi kuacha dhana potofu juu ya magonjwa yanayotambulika hospitalini.

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji