Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baba ashikiliwa kwa mauaji ya mke na mtoto

Jumamosi , 17th Apr , 2021

Jeshi la Polisi mkoani Kagera linamshikilia Joachim Rwegasira mwenye umri wa miaka 45 mkazi wa kitongoji cha Rushonga kata Buganguzi wilayani Muleba kwa tuhuma za kuwaua mke na mtoto wake mdogo mwenye umri wa mwaka mmoja, kwa kuwakata na kitu chenye ncha kali.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Maketi Msangi

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Maketi Msangi amesema kuwa tukio hilo limetokea Aprili 16 mwaka huu saa tisa Alasiri, na kuwataja waliouawa kuwa ni Rosemary Joachim mwenye umri wa miaka 35 na mtoto wake Joiness Joachim mwenye umri wa mwaka mmoja.

Msangi amesema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa kimapenzi na kwamba baba huyo amekuwa akimlalamikia mke wake kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na jirani yao na kwamba hata mtoto huyo alimzaa na jirani, ambapo baada ya kutekeleza mauaji hayo mtuhumiwa huyo alijaribu kujiua bila mafanikio.

"Mtuhumiwa alijikata kwa kitu chenye ncha kali sehemu za tumboni katika kitovu na shingini akilenga kujidhuru lakini hakufanikiwa na  alikamatwa akiwa hai", amesema.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda huyo, mtuhumiwa huyo amelazwa katika hospitali teule ya wilaya ya Muleba iitwayo Rubya, kwa matibabu na hali yake sio nzuri.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa