Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baba jitu zima lahukumiwa miaka 30 jela kwa kubaka

Jumatatu , 25th Jul , 2022

Marwa Nyamuhanga (33) mkazi wa Nyabisare Halmashauri ya Manispaa ya Musoma, mkoani Mara amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma kwa kosa la kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka saba.

Marwa Nyamuhanga, aliyehukumiwa miaka 30 jela

Akisoma hati ya mashtaka mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma, Hakimu Mkazi Mwandamizi Stanley Mwakihaba, Mwendeshesha mashtaka mwanadamizi wa serikali Monica Hokororo, amesema mshtakiwa huyo anakabiliwa na kesi ya jinai no 7 ya mwaka 2022 ikiwa ni kinyume na kifungu cha Sheria no.130 (1),2 (e) na kifungu cha 131 (1) cha kanuni ya adhabu kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2019.

Hokororo amesema mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo Desemba7, 2021, katika eneo la Nyabisare ambapo mtuhumiwa alimwita mtoto huyo na kumpatia shilingi 500 na kumtuma akamnunulie maandazi na kisha kumwingiza katika pagala la nyumba na kuanza kumtendea unyama huo ambapo alitimiza adhima yake ya ubakaji.

Mwendesha mashitaka ameendelea kuambia Mahakama hiyo kuwa mshtakiwa huyo wakati akiendelea kumbaka mtoto huyo mtoto alikuwa akipiga kelele za kuomba msaada ndipo dada wa muathiriwa na mama yake walifika eneo la tukio na kumkuta kijana huyo Marwa akiwa anatenda tendo hilo la ubakaji.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mwandamizi Stanley Mwakihaba, amesema Mahakama hiyo imethibitisha pasi kuacha shaka ya aina yoyote kwa mshtakiwa huyo kuwa ametenda kosa hilo la ubakaji.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava