Ubakaji
Valentina Mkolongo ni Mama mzazi wa mtoto aliyebakwa ambaye pia ana jumla ya watoto watano amesema kwa muda mrefu amekuwa na mgogoro na mume wake na ikafika wakati akafukuzwa chumbani na kulazimika kuhamia chumba kingine, na moja ya chanzo cha mgogoro ni mama kupinga uhusiano uliokuwa unatia mashaka kati ya Baba na Binti yao wa kwanza mwenye umri wa miaka 11.
Kwa upande wake mtoto ambaye anadaiwa kubakwa na Baba yake mzazi amesema wakati wakulala alikuwa akiwaita yeye na wadogo zake na wakiwa wamelala akawa anatumia muda huo kumbaka.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Kamishna Msaidizi wa Polisi Hamis Issa, amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa ambaye ni mfanyabiashara wa Mkaa.