Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bado tunamshikilia Zitto Kabwe - Kamanda Matei

Ijumaa , 23rd Feb , 2018

Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe bado anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro toka jana (Alhamisi) kwa tuhuma za kufanya mkusanyiko bila ya kuwa na kibali.

Hayo yameelezwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Ulrich Matei  na kudai wanaendelea na mahojiano nae ili waweze kufahamu alitoa wapi taarifa ya kufanya mkutano ya chama katika maeneo ya nje pamoja na kujua kitu alichokuwa anazungumza na wananchi wa Kata ya Kikeo iliyopo wilayani Mvomero ambapo ndipo alipokamatiwa.

"Ni kweli bado tunamshikilia Zitto Kabwe, tuna muhoji kwa sababu ya kufanya mikutano bila ya kuwa na kibali. Amekwenda kufanya mikutano ya nje maeneo ya hapa Mgeta katika Kata ya Kikeo iliyopo wilayani Mvomero", amesema Kamanda Matei.

Pamoja na hayo, Kamanda Mtei ameendelea kwa kusema "haikuwa inajulikana anazungumzia kitu gani katika mkutano wake, sasa tunajaribu kumhoji ili kuweza kufahamu mazingira yale aliendaje kule na labda alitoa taarifa sehemu gani. Mpaka sasa hivi yupo polisi na suala la dhamana lipo wazi tu anaweza kudhaminiwa muda wowote".

Mbunge Zitto Kabwe pamoja na viongozi wengine wa ACT- Wazalendo tokea  Februari 19 wapo katika ziara ya mikoa nane yenye kata zinazoongozwa na chama hicho kwa malengo ya kushiriki kazi za maendeleo na kuzungumza na kamati za maendeleo za kata hizo.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava