Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bajeti ya 2019/20 yawasilishwa na haya mapendekezo

Alhamisi , 13th Jun , 2019

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amesoma makadirio ya Bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/2020, bungeni leo Juni 13, 2019.

Waziri wa Fedha Dkt. Philip Mpango

Katika makadirio hayo Waziri mpango amesema jumla ya shilingi Tril 33.11 zinatarajiwa kukusanywa na kutumika katika bajeti ya mwaka 2019/20.

''Mapato ya ndani ni Tril 23.05 ambayo ni 69.6% ya bajeti yote. Mapato yatakayotokana na kodi ni Tril 19.10 sawa na asilimia 12% ya pato la taifa'' - Philip Mpango.

Baadhi ya michanganuo ya bajeti 2019/2020

Tril 7.56 Mishahara,
Tril 1.44 Umeme vijijini,
Bil 788.8  Reli, Maji, Usambazaji Umeme
Bil 450 Elimu ya juu
Bil 288.5 Elimu bure,
Bil 600 Wazabuni

Katika bajeti hiyo Waziri Mpango pia amependekeza kufutwa kwa msamaha wa kodi kwenye taulo za kike.
''Kufuta kwa msamaha kodi ya ongezeko la thamani kwenye taulo za kike kwa kuwa haujawezesha kupatikana kwa bei nafuu kwa bidhaa hiyo muhimu kwa walengwa, badala yake ni kuwanufainisha wafanyabiashara'', amesema.

Aidha amependekeza kutoza ushuru wa asilimia 10 kwenye bidhaa za nywele za bandia, zinazotengenezwa ndani ya nchi na asilimia 25 zinazoagizwa kutoka nje ya nchi, lengo ni kuongeza mapato ya Serikali.

Pia amependekeza kuongeza muda wa leseni ya udereva kutoka miaka 3 hadi 5, kuongeza tozo ya leseni 40000 hadi 70000, ada ya usajili wa magari 10000 hadi 50000, bajaji kutoka 10000 hadi 30000 na pikipiki kutoka 10000 hadi 20000.

Amesisitiza kuwa tozo zote zilizokuwa zinatozwa kwa dola za Kimarekani zitatozwa kwa shilingi ya Tanzania, isipokuwa kwa shehena za kemikali zinazokwenda nje ya nchi.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava