Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

BAVICHA wamshtua Jaji Mkuu

Jumatano , 20th Feb , 2019

Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) limelaani nguvu kubwa inayotumiwa na Jeshi la Polisi mahakamani wakati wa usikilizwaji wa kesi za viongozi wa chama hicho jambo ambalo wamemtaka Jaji Mkuu kuzisimamia mahakama zitende haki.

Mwenyekiti wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi

Mwenyekiti wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi amesema hayo leo Februari 20, 2019 licha ya Desemba, 2018 kumuandikia barua Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma bado kuna ukiukwaji wa haki mahakamani.

Sosopi, ameeleza kwamba  Februari 18, 2019 wakati wa usikilizwaji wa rufaa ya Mwenyekiti Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini,  Esther Matiko, baadhi ya wanachama walikamatwa na wengine kupigwa walipojitokeza kufuatilia mwenendo wa kesi hiyo.

"Mahakama ni mhimili unaojitegemea na sehemu huru kila mtu anapaswa kwenda kusikiliza kesi kama polisi wakiendelea kuingilia mhimili huu tutegemee mahakama zetu kugeuka mahakama za kijeshi," ameeleza.

"Tulimuandikia barua Jaji Mkuu Desemba 12, 2018 kumweleza ukiukwaji wa haki unaofanywa mahakamani lakini bado vitendo hivi vimeendelea kutia doa mhimili huo, na juzi uvunjifu wa haki umefanyika nje ya ofisi yake, vijana wetu wengine walipigwa, wwengine walichukuliwa na kurudishwa muda wa mahakama ukiwa umeisha ,"  Sosopi ameongeza.

Pia baraza hilo limelaani na kusikitishwa na mauaji yanayoendelea kutokea maeneo mbalimbali nchini ikiwemo watu kufa wakiwa mikononi mwa jeshi polisi.

"Kumekuwa na mauaji yanayotokea maeneo mbalimbali Serikali imeshindwa kukomesha mauaji hayo na badala yake tunaendelea kusikia watu wanafia mikononi mwa jeshi la polisi.

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji