Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

BAWACHA wamjibu Spika Ndugai  

Jumanne , 4th Mei , 2021

Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, BAWACHA limekanusha madai ya kuwa chama chao kina mfumo dume, kwa kusema kuwa chama hicho ndicho chama pekee chenye wajumbe wengi wanawake.

Mjumbe Kamati Kuu Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Suzan Kiwanga

Akizungumza leo na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam, Mjumbe Kamati Kuu CHADEMA, Suzan Kiwanga, mara baada ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai kuagiza Katibu Mkuu CHADEMA kuandika barua ambayo ataambatanisha na katiba ya chama na muhtasari wa kikao kilichofanya maamuzi ya kuwafukuza uanachama wabunge 19 wa chama hicho, amesema BAWACHA watashughulikia suala la wabunge hao kwa mujibu wa katiba.

“Chama chetu hakina mfumo dume kama ambavyo inasambazwa huko, sisi ndio chama pekee chenyewe wajumbe wengi wanawake Kamati Kuu kuliko chama chochote cha Siasa Tanzania, Chama chetu ndio kilikuwa na wagombea wengi wanawake majimboni, ambapo tulikuwa zaidi ya 60 majimboni tofauti na chama chochote” amesema  Suzan Kiwanga

Wakiongelea suala la wabunge 19 na yale yaliyobainishwa na Spika Ndugai BAWACHA wameeleza kushangazwa na mkinzano uliopo katika ofisi ya spika kutokana na kutofautiana kwa taarifa, huku wakiendele kusema kuwa CHADEMA haiwatambui wabunge hao.

“Wakati Spika anawaondoa Bungeni waliokuwa Wabunge wa CUF Bunge lililopita Spika hakuomba hivyo vielelezo anavyoviomba kwetu, ametukosea sana kuita barua yetu kipeperushi, Hao anaowaita Wabunge sisi hatuwatambui tunawaona wasaliti tu katika Chama, tuliwaita kwenye kikao cha Kamati Kuu tuwasikilize lakini hawakutokea” amesema  Suzan Kiwanga

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava