Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

CHADEMA wanagawa fedha na sukari - Polepole

Ijumaa , 14th Sep , 2018

Chama cha Mapinduzi (CCM), kimesema uchaguzi mdogo wa marudio unaotarajiwa kufanyika Septemba 16, 2018 umekuwa uchaguzi wenye mtihani kwao, kwa madai kukiukwa kwa baadhi ya sheria za uchaguzi ya mwaka 1985 kutoka wapinzani wao wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Katibu wa Itikadi wa Uenezi Humphrey Polepole

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Katibu wa Itikadi wa Uenezi Humphrey Polepole amesema wapinzani wao wamekuwa wakitumia lugha zisizo na staha pamoja na utoaji wa rushwa kwenye mikutano ya kampeni unaofanywa na baadhi ya viongozi wake.

Polepole amesema "wenzetu hawakutaka kuheshimu sheria za vyama vingi, hawakufata maadili ya uchaguzi wenzetu wameyapuuza yote.., kinyume na sheria ya uchaguzi ya mwaka 1985, niwaambie tu TAKUKURU, chama cha CHADEMA wanagawa fedha na sukari kule Monduli na tunalifahamu hilo, tunaomba lifuatiliwe".

Polepole akaongeza, "Kamati ya maadili ya uchaguzi ya jimbo la Ukonga ilitoa adhabu kwa viongozi wa CHADEMA waliotumia lugha chafu kwenye kampeni ikiwemo kumtukania utu wake Mwita Waitara, ikiwataka waombe radhi hadharani lakini wamekaidi mpaka sasa".

Katika hatua nyingine Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM amesema licha ya changamoto hizo wana uhakika kuwa chama chao kitashinda chaguzi hizo.

Uchaguzi wa majimbo ya Monduli  na Ukonga unarudiwa kutokana waliokuwa wabunge wake kwa tiketi ya CHADEMA, Julius Kalanga kwa upande wa Monduli na Mwita Waitara kwa upande wa Ukonga kujiuzulu huku wakiwania tena nafasi hiyo kupitia CCM.

Katika chaguzi hizo Tume ya Uchaguzi ilitangaza marudio ya uchaguzi katika kata 20 pamoja na majimbo matatu ikiwemo jimbo la Korogwe vijijini ambalo mgombea wake Timotheo Mzava wa CCM alipita bila kupingwa na pia katika kata chaguzi za kata 20 chama hicho kilipita bila kupingwa kwa kata 12.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava