Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chadema yapata pigo

Jumatano , 26th Jul , 2017

Diwani wa kata ya Moita wilayani Monduli (CHADEMA) Edward Sapunyo amesema sababu ya kujiuzulu uongozi ni kutokana na vikwazo vilivyowekwa na chama chake wakati wa kufanya kazi na watendaji wa serikali, kitendo ambacho kinatafsiriwa kama  usaliti.

Moita ambaye amewawakilisha viongozi wengine wanaoendelea kujiuzulu mkoani Arusha wamesema wanalazimika kuchukua hatua hiyo kutokana na kunyimwa fursa ya kushirikiana na viongozi na watendaji wa serikali kutatua kero za wananchi ikiwa ni pamoja na kutaka kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kazi anayoifanya.

Moita amesema anachokijua yeye ni kwamba pamoja na kuwa kiongozi kwenye chama cha Upinzani anapaswa kushirikiana na watendaji waliopo madarakani kutatua kero za wananchi lakini baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani wamekuwa wakiona kama ni usaliti.

“Moja ya jambo lililoniuma kuna mradi wa maji ambao nimehangaika nao tangu mwaka 2006 fedha zilipatikana na umekuwa unaendelea vizuri, lakini viongozi wangu wanaukwamisha usifikie tamati licha ya kuwa wananchi wameanza kutumia maji,”  alisema

Hata hivyo baadhi ya wananchi wa kata hiyo wametofautiana mitazamo juu ya kujiuzulu kwa madiwani hao ambapo baadhi yao wamefurahia na wengine wamesema wanachotaka ni kuona matatizo yao yanapata ufumbuzi na wanakuwa na maendeleo.

Kiongozi huyo amekabidhi barua yake ya kujiuzulu jana na kufikisha idadi ya madiwani waliojiuzulu mkoani Arusha kufika tisa.

 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine