Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

CHADEMA yatoa tamko kuhusu 40 walikamatwa

Jumatano , 21st Feb , 2018

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara na Mbunge wa Kibamba, John Mnyika amelitaka Jeshi la Polisi nchini kutoa kauli juu ya watu 40 waliokamatwa kwenye maandamano ya chama hicho Februari 16, 2018 katika eneo la Magomeni Jijini Dar es Salaam.

Mnyika ameeleza hayo jioni ya leo wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupita takribani siku tano tokea kwa watu hao kukamatwa na kuweka ndani ambapo amedai endapo Polisi wakishindwa kuwapa dhaman na kuwatolea ufafanuzi hadi ifikapo kesho basi wapelekwe Mahakamani.

"Jeshi la Polisi mpaka hivi sasa wamekwisha vunja sheria kwa kutowapa dhamana wala kuwafikisha Mahakamani. Tunalitaka Jeshi la Polisi kupitia kwa IGP na Kamanda wa Kanda maalumu ya Dar es Salaam, kutoa kauli leo juu ya hao ambao wanawashikilia na kuwanyima dhamana na kutowafikisha Mahakamani", amesema Mnyika.

Pamoja na hayo, Mnyika ameendelea kwa kusema "Jeshi la Polisi litoe tamko kwa kuidhinisha kwa majina watu wote 40 na kama kuna wengine vile vile wanawashikilia wawataje kwa majina na waeleze taratibu za kuwapa dhamana ya kipolisi na kama hawawezi hilo basi kesho asubuhi wawapeleke Mahakamani ili waweze kupewa haki yao".

Kwa upande mwingine, Mnyika amedai kwa mujibu wa taarifa walizokuwa nazo Jeshi la Polisi liliwakamata watu wengine ambao walikuwa wanajishughulisha na shughuli zao huku wengine wakiwa wametoka kushuka kwenye madaladala.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto