Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chalinze Modern Islamic yateketea

Jumatano , 6th Jul , 2022

Moto mkubwa umezuka ghafla na kuteketeza moja ya bweni lililopo katika shule ya msingi ya Chalinze Modern Islamic iliyopo Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani na kuathiri miundombinu ya bweni hilo ikiwemo vifaa vya kusomea na nguo za wanafunzi shuleni hapo 

Inaelezwa kuwa moto huo ulizuka wakati ambao wanafunzi walikua msikitini wakiswali swala ya alfajiri.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa kikosi cha zimamoto mkoa wa Pwani Jenifa Shirima amesema alipata taarifa za kuzuka kwa moto huo majira ya saa kumi na moja na dakika 42 alfajiri na kufika shuleni hapo ambapo walifanikiwa kuuzima moto huo kwa kushirikiana na uongozi wa shule watumishi pamoja na wanafunzi ambao hivi karibuni walipatiwa mafunzo ya namna ya kukabiliana na majanga kama hayo.

Nae mkuu wa mkoa wa Pwani Alhaj Aboubakari Kunenge akizungumza mara baada ya kufika katika eneo la tukio amesema licha ya ajali hiyo kuteketekeza vibaya bweni la wavulana katika shule hiyo zikiwemo zana mbalimbali za kujisomea lakini hakuna mwanafunzi yeyote alidhurika kufuatia moto huo kwani wakati unazuka wanafunzi walikuwa msikitini wakiswali swala ya alfajiri.

Hili ni tukio la pili la ajali ya moto kuteketeza bweni ambapo mnamo mwezi Mei mwaka huu tulishudia bweni la sekondari ya wasichana Mkuza iliyopo Kibaha Pwani mali ya kanisa la KKKT likiteketea kwa moto wakati wanafunzi wakiwa katika ibada
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava