Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chiza arudi tena Buyungu

Jumatatu , 13th Aug , 2018

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imemtangaza Mhandisi Christopher Chiza kutoka CCM kuwa mshindi wa kiti cha Ubunge katika Jimbo la Buyungu Mkoani Kigoma baada ya kupata jumla ya kura 24,758 akifutiwa na Elias F. Michael aliyepata kura 16,910 kutoka CHADEMA.

Mhandisi christopher Chiza

Hayo yamebainishwa na msimamizi wa uchaguzi jimboni humo Lusubilo Mwakabibi ambapo amesema watu waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 61,980 na kura zilizopigwa zilikuwa 42,356 huku zikiharibika kura 515.

Matokeo hayo yametokana na uchaguzi mdogo wa marudio uliofanyika jana Jumapili Agosti 12, 2018, katika Mkoa huo kufuatilia jimbo hilo kuwa wazi.

Licha ya matokeo hayo kutangazwa, mgombea kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), amedai hakutendewa haki kutokana na kunyimwa baadhi ya fomu za matokeo na kutokubaliwa kuingia katika chumba cha kuhesabia kura, huku akidai zaidi kuwa yeye alishinda kwa kura 22,000 huku Chiza akiwa amepata kura 18,000.

Kwa upande wake mshindi wa nafasi kiti hicho cha Ubunge, Mhandisi Christopher Chiza amewashukuru wananchi wa Kigoma kwa kuweza kumuamini kuwa mwakilishi wao Bungeni kwa mara nyingine tena.

Mhandisi Chiza ambaye ni mshindi wa jimbo hilo kwa sasa pia aliwahi kulitumikia jimbo hilo kwa takribani miaka 10 iliyopita, kuanzia mwaka 2005 hadi 2015 kupitia CCM, ambapo alikuja kuangushwa katika uchaguzi wa Rais na Wabunge wa mwaka 2015  na marehemu Kasuku Bilago aliyekuwa CHADEMA.

Mnamo Julai 10, 2018, Katika kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichokuwa kinaongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa ambaye pia ni Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, walimteua Mhandisi Christopher Kajoro Chiza kuwa mgombea wa Ubunge katika Jimbo la Buyungu.

Uchaguzi huo wa marudio umefanyika baada ya kufuatia aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia tiketi ya Chadema, Kasuku Samson Bilago kufariki dunia mnamo Mei 26, 2018, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alikokuwa amelazwa kwa matibabu na kupelekea jimbo hilo kuwa wazi.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto