Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Aboubakar Kunenge
Kunenge ameyasema hayo alipofanya ziara ya kukagua miradi minne ya maendeleo Jijini humo ambapo amemtaka mkandarasi huyo kuhakikisha ujenzi inakamilika kabla ya Mwezi Oktoba.
''Taasisi za DAWASA na TANESCO fanyeni kazi kwa ushirikiano na mkandarasi ili asipate kisingizio chochote cha kuchelewesha kazi hii inayotakiwa kukamilika Oktoba,'' amesema.
Aidha Mkuu huyo wa mkoa amesema barabara hiyo yenye urefu wa Km 4.5 ni moja ya barabara muhimu katika kutatua changamoto ya foleni kwenye barabara ya Bagamoyo, ambapo mradi huo umegharimu zaidi ya Bilioni 8.2.