Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dkt. Mpango awapa onyo watumishi wa umma wezi 

Jumatatu , 26th Jul , 2021

Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philip Mpango ametoa onyo kali kwa watumishi wa umma wanaofanya vitendo vya wizi wa mali na vifaa vya umma na kusema kuwa kwa yeyote atakayebainika kuhusika na wizi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake

Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philip Mpango (watatu kushoto) akiweka
jiwe la msingi Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini iliopo Manispaa ya Mikindani mkoani Mtwara, Julai 26,2021.

Dkt Mpango ametoa onyo hilo leo, wakati akiweka jiwe la msingi la Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini Mtwara, lililojengwa na NHC kama Mkandarasi, na kusema kuwa hatokuwa mpole wala kuchekea wizi wa mali na vifaa vya umma.

“Natanguliza onyo kali kwa watumishi wasiowaaaminifu katika sekta ya afya na hasa upande wa manunuzi kwenye bohari yetu ya dawa, idara za tehema, maduka ya dawa niwaambie serikali ya awamu ya sita itachukua hatua kali sana kwa yeyote atakayefanya uzembe au kuhusika na wizi dawa,” amesema Dkt. Mpango.

 “Mtumishi yeyote tutayembaini amehusika na wizi wa dawa na vifaa vyake, Mhe Naibu Waziri wa Afya kamwambie Katibu mkuu wako, cha kwanza muondeeni kazini tumechoka na msiishie hapo vyombo vya sheria vipo apelekewe Mahakamani, niwaambie kabisa tutataifisha chochote alichonacho ili kufidia upotevu wa dawa zetu,” ameongeza Dkt. Mpango.

Samabamba na hilo Dkt. Mpango ameendelea kuwasihi wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya janga la corona kwani wimbi la sasa linauwa haraka zaidi.

“Ugonjwa wa corona upo, tulifanya vizuri sana tulipopigwa na wimbi la kwanza na la pili baada ya hapo tukaona Mungu ameshalifukuzilia mbali tukajisahau, limekuja wimbi la tatu baya zaidi hata dalili zake zinatofautiana, linaua haraka zaidi,” amesema Makamu wa Rais Dkt. Mpango.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava