Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Fahamu matarajio ya wakenya kwa Rais Samia

Jumanne , 4th Mei , 2021

Wakili Msomi nchini Kenya, Prof. George Wajackoyah amesema kitendo cha mabunge mawili kuungana kumpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye anatarajia pia kuhutubia bunge nchini humo  ni heshima kubwa kwake kwani hutokea mara chache.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan

Akizungumza kwenye mahojiano na Kipindi cha Supa Breakfast, cha East Africa Radio, Prof. Wajackoyah amesema miaka miwili iliyopita Waziri Mkuu wa Uingereza alikaribishwa nchini Kenya, lakini hakupata nafasi hiyo ya kuhutubia mabunge yote mawili nchini Kenya.

"Rais Samia atahutubia mabunge yote kwa pamoja hiyo ni heshima kubwa kwa Rais wa Tanzania, kwani hata miaka miwili iliyopita Waziri Mkuu wa Uingereza aliwahi kukaribishwa nchini Kenya, lakini hakuhutubia mabunge yote mawili" amesema Prof. Wajackoyah

Akielezea matamanio ya wananchi wa Kenya, Prof. Wajackoyah ameeleza kuwa wamefurahishwa na ujio huo huku wakimuomba Rais Samia kushirikiana na wapinzani wake katika siasa ili kukuza uchumi na amani ya nchi.

"Watu wamefurahi na wanauliza alisema ataweza kuleta uhusiano mwema kati ya nchi jirani, wamesema wangefurahi sana ikiwa mama Samia angeweza kuhusiana na wapinzani wake wa siasa ili waijenge Tanzania iwe nchi ya amani, Na kuna wale vibaraka hawataki mama aongee na majirani zao ingekuwa vizuri akaanza kujadiliana na wapinzani wa siasa kuleta uchumi, uhusiano mwema na ujirani mwema" amesema Prof. Wajackoyah

HABARI ZAIDI

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe