Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Gari la Mkuu wa mkoa wa Mara lagongeshwa na mtoto

Jumatatu , 5th Aug , 2019

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara RPC Juma Ndaki,  amesema hali ya gari la Mkuu wa Mkoa huo Adam Malima, hairidhishi kabisa hii ni baada ya gari hilo kugongeshwa na mtoto wa dereva na kuharibika vibaya.

Gari hilo baada ya kupata ajali

Gari hilo lenye namba STL 5962 liligongeshwa jana Agosti 4, 2019, maeneo ya Kwangwa Musoma mjini na mtoto anayedhaniwa kuwa ni wa dereva wa Mkuu wa Mkoa, baada ya kulichukua bila ridhaa ya baba yake na kuondoka nalo.

''Gari hiyo aliiacha kwenye silencer ili akitoka mgeni airudishe kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa, lakini wakati anaongea na mgeni yule mtoto akaingia ndani ya gari nakuondoka nayo, sasa katika uendeshaji ikamshinda ikawa imetoka nje ya barabara na kugonga daraja,  ikawa imehabribika kwa kiasi kikubwa, na mtoto kakimbizwa hospitali kutokana na majeraha aliyoyapata'' amesema RPC Ndaki.

Kufuatia ajali hiyo kijana huyo amelazwa hospitali kutokana na kuumia sehemu ya kifua na mkono, ambapo baada ya dereva ( Baba yake) kukuta hali ya gari si nzuri na yeye alipata mshituko na kuanguka na kupelekwa hospitali.

Aidha Kamanda Ndaki amesema kuwa Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi, na kwamba watawachukulia hatua stahiki wote waliosababisha ajali hiyo akiwemo dereva aliyeacha gari na kisha kuchukuliwa kizembe.
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA