Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Halima Mdee kujitetea mahakamani

Jumamosi , 15th Aug , 2020

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam Septemba 7, 2020 itasikiliza utetezi katika kesi ya uchochezi inayomkabili aliyekuwa Mbunge wa Kawe (CHADEMA), Halima Mdee.

Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA, Halima Mdee

Kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa mahakamani hapo Agosti 12, 2020 lakini ilishindikana kwa kuwa mawakili wa utetezi hawakufika mahakamani. 

Mdee alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, kuwa mawakili wake, Peter Kibatala na Hekima Mwasipu hawakuwepo mahakamani hapo kwa sababu walikuwa kwenye kesi nyingine Mahakama Kuu Kitengo cha Biashara na Kazi.

Awali, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai kuwa shauri hilo liliitwa kwa ajili ya mshitakiwa kuanza kujitetea. Simon alidai kuwa kwa kuwa mawakili wa mshitakiwa huyo hawakuwepo mahakamani hapo aliiomba Mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya utetezi.

Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 7, 2020 kwa utetezi, Mdee anadaiwa kuwa Julai 3, 2017 katika ofisi za makao makuu ya CHADEMA mtaa wa Ufipa wilayani Kinondoni, alitenda kosa la kutoa lugha chafu.

Inadaiwa kuwa Halima alitamka maneno machafu dhidi ya Rais John Magufuli na kwamba kitendo hicho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali