Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Hata Mwalimu aliwachapa kina Sitta Ikulu"- Wasira

Jumatatu , 14th Oct , 2019

Aliyewahi kuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Stephen Wasira amezungumza jinsi kipindi cha miaka 7 ya Ukuu wa Mkoa wa Mara ulivyomsaidia kumfahamu vizuri hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Stephen Wasira

Wasira ameyabainisha hayo leo Oktoba 14, 2019, wakati wa Kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa, lililofanyika Kijijini Butiama mkoani Mara.

''Kama kuna wakati nimejifunza juu ya maisha ya Mwalimu ni katika kipindi cha mika 7 na nusu ya Ukuu wa Mkoa wa Mara kwasababu alikuwa anakuja hapa kila Pasaka na Christmas, anakaa sana na kiserikali mimi ndiye nilikuwa mwenyeji wake, Mwalimu alikuwa anasikiliza sana hata kama unaongea vitu vya hovyo hovyo anakusikiliza na wala hakuambii ukae'', amesema Wasira.

Aidha Wasira amelizungumzia suala la Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila la kuwachapa Wanafunzi viboko akisema kuwa hata Mwalimu aliwahi kufanya hivyo kwa kina hayati Samuel Sitta walipokuwa wanafunzi wa Chuo Kikuu.

''Nchi inaendeshwa kwa utaratibu, kama utaratibu ni viboko wanachapwa tu, maana hata Mwalimu alishawahi kuwachapa kina Sitta viboko pale Ikulu, wakiwa Wanafunzi wa Chuo Kikuu, walijifanya vituko aliwachapa mwenyewe, aliuvua Urais akawa Mwalimu, inategemea hali ilivyo kwa wakati huo'', ameongeza.

Wasira ameendelea kumsifia Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, kwamba alikuwa ni mtu anayechukia umaskini na hakutaka huo utajiri awe nao peke yake na kwamba kama angetaka hivyo huenda ndiyo angekuwa ni tajiri mkubwa Afrika na Duniani.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava