Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Hatujazuiliwa kukutana, uchaguzi upo" - JPM

Alhamisi , 26th Mar , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amesema kuwa vikao vya kawaida vya watendaji wa Serikali vitaendelea na hata Uchaguzi Mkuu utafanyika kama ilivyopangwa.

Rais Magufuli

Amesema hayo leo, Machi 26, 2020 katika hafla ya kupokea ripoti kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali CAG na ripoti ya TAKUKURU katika Ikulu ya Chamwino Jijini Dodoma.

Rais Magufuli amesema kuwa hata nchi ambazo zimeathirika zaidi na virusi vya Corona, bado mabunge na mabaraza yao yanaendelea na kusema kuwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utafanyika.

"Hatujazuiliwa kukutana, leo nimesoma gazeti moja linasema 'Madiwani wafanya kikao cha Madiwani', sijui alifikiri vikao vya madiwani vimezuiliwa kwa sababu ya Corona?. Sisi tunaendelea kukutana katika mikutano hii ya kawaida na hata Bunge ndio maana linaendelea", amesema Rais Magufuli.

"Kazi lazima iendeleea kufanyika na uchaguzi tutafanya tu, wapo wengine wanafikiri nitaahirisha, ni nani anataka kukaa kwenye maofisi haya muda wote huu", ameongeza Rais Magufuli.

Katika ripoti ya ukaguzi iliyowasilishwa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG, Charles Kichere, jumla ya hati 1084 za Taasisi za Serikali Kuu, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Mashirika ya Umma, miradi ya maendeleo na Vyama vya Siasa kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2019 zimekaguliwa. Hati zinazoridhisha ni 1017, zenye shaka ni 46, hati zisizoridhisha ni 7 na hati mbaya 12. 

Pia Rais Magufuli amempandisha cheo aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali, John Mbungo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo kwa kazi nzuri aliyoifanya ikiwemo ya kurejesha bilioni 8.8 walizodhulumiwa wananchi.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava