Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Hii rekodi imevunjwa na Magufuli pekee

Alhamisi , 5th Nov , 2020

Unaweza kusema kuwa Rais John Pombe Magufuli, amekuwa Rais mwenye bahati ya aina yake katika hafla ya kuapishwa kwake iliyofanyika leo Novemba 5 katika viunga vya Uwanja wa Jamhuri, Jijini Dodoma kutokana na kutengeneza kurasa mpya za historia ambazo hazikuwahi kutokea hapo kabla.

Pichani ni Rais Dkt John Magufuli akiwa amebeba Ngao na Mkuki, kuashiria kukabidhiwa hatamu za uongozi.

Magufuli baada ya kuapishwa alitoa hotuba fupi ambayo sehemu yake ilieleza adhma ya serikali yake pamoja na mambo mengine kuwa ni kuwaletea wananchi maendeleo, usimamizi bora wa rasilimali pamoja na kuimarisha uchumi.

Miongoni mwa rekodi ambazo Magufuli amezivunja ni pamoja na kuapishwa leo tarehe 5 Novemba 2020 sawia na tarehe ambayo alipishwa katika muhula wa kwanza mwaka 2015.

Rekodi nyingine ni kuwa Rais wa kwanza barani Afrika kutosafiri nje ya bara hilo tangu tarehe ya kuapishwa katika muhula wa kwanza hadi tarehe ya kuapishwa katika muhula wa pili.

Pia Magufuli anakuwa Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuapishwa nje ya Jiji la Dar es Salaam na wa kwanza katika Jiji la Dodoma yaani Makao Makuu ya nchi na serikali. Pia kuwa Rais wa kwanza kula kiapo cha Urais, Taifa likiwa katika uchumi wa kati.

Rekodi nyingine ni pamoja na kuwa Rais wa kwanza nchini kushinda kinyang'anyiro cha Urais kwa asilimia ndogo zaidi katika muhula wake wa kwanza na kupata kura nyingi zaidi katika mbio za kusaka muhula wake wa pili (Magufuli 2015 kura 8,882,935 sawa na 58.46% na 2020 kura 12,516,252 sawa na 84%) tofauti na watangulizi wake.

Lakini Magufuli historia inamfananisha na Marais wenzake waliomtangulia mathalani katika eneo la kushinda mihula miwili katika nafasi ya Urais tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini 1992 ambapo Marais waliomtangulia ni pamoja na Benjamini Mkapa (1995-2005), Jakaya Kikwete (2005-2015).

 

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine