Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jaji Mkuu aapishwa, atoa neno

Jumatatu , 11th Sep , 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo amemuapisha Prof. Ibrahim Hamis Juma kuwa Jaji Mkuu, ambaye alimteua kushika wadhifa huo Septemba 10, mwaka huu.

Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Juma akiwa Rais Magufuli.

Katika hafla hiyo ambayo imefanyika Ikulu jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa kitaifa wakiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Mh. Job Ndugai na Majaji wengine wa Tanzania, Jaji Ibrahim Juma amesema anashukuru kwa kurasimishwa kushika wadhifa huo ambao alikuwa ana ukaimu takriban miezi nane mpaka alipoteuliwa kuwa Jaji Mkuu.

Katika hotuba yake ya kwanza Jaji Mkuu Ibrahim Juma ameahidi kuitumikia nafasi hiyo kwa weledi ikiwemo kulinda sheria na kuweka imani kwa wananchi, kwani wao ndiyo watetezi wao.

"Jambo ambalo ni muhimu kwetu sisi katika kufanya kazi ni kuhakikisha kwamba tunaendelea kuwa na imani ya wananchi, kwa sababu wananchi wasipokuwa na imani na mahakama pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama hawatakuja kwetu ili kutatua matatizo yao", alisema Jaji Mkuu Ibrahim Juma.

Jaji Ibrahim ameendelea kusema kwamba "tumejiwekea mipango ya kuhakikisha tunaendelea kupata imani ya wananchi wetu, na tutafanya hivyo kwa kuepuka utovu wa maadili, vitendo vya rushwa na ucheleweshaji wa mashauri".

Ibrahim Juma alianza kutumikia wadhifa wa Kaimu Jaji Mkuu tokea Januari 18 mwaka 2017, baada ya aliyekuwa Jaji Mkuu wa nchi Mheshimiwa Mohamed Chande Othman kustaafu.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava