Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jela kwa kumuua aliyemimina pombe

Alhamisi , 31st Mar , 2022

Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Kigoma imewahukumu jela miaka miwili, watu wawili Tumaini Thomas na Jonas Mbilimi, wakazi wa Nyachenda wilayani Kasulu baada ya kumuua mwenzao aliyemimina pombe yao ya kienyeji aina ya Wanzuki wakiwa wanalewa kwenye kilabu cha Pombe.

Picha ya mfano wa mtu anayemimina pombe ya kienyeji

Kesi ya mauaji ya bila kukusudia namba 14 ya mwaka 2021 Jamuhuri dhidi yao ikisikilizwa na jaji mfawidhi wa mahakama hiyo Lameck Mlacha, mnamo Septemba 5, 2020 washtakiwa wakiwa wanakunywa pombe  marehemu akanyanyuka na kumimina pombe hiyo hali iliyosababisha ugomvi na  marehemu alikimbia wakamuangusha na kumkanyaga na miguu pamoja na kumpiga na kigoda kichwani.

Upande wa Jamuhuri uliwasilisha ushahidi mashuhuda wa tukio hilo, Askari na ndugu pamoja na ushahidi wa daktari ulio eleza  fuvu la kichwa upande wa kushoto lilivunjika na kifo kilisababishwa na kuvuja damu nyingi kwenye ubongo.

Upande wa utetezi ukiwakilishwa na wakili Joseph Mathias washtakiwa walisema walikuwepo wakati wa tukio na ugomvi ulivyoibuka mmoja wao aliamua ili wasigombane kisha wakaenda nyumbani na baadae kupata taarifa ya kifo hicho.

Jaji Mlacha baada ya kuangalia ushahidi wa pande zote amesema washtakiwa wameidanganya mahakama kwa kuwa mashahidi walio kuwepo walishuhudia tukio pamoja na maelezo ya marehemu kwa familia kabla hajafa hivyo ikawakuta na hatia ya mauaji ya bila kukusudia na wakili wa Jamuhuri Benedict Kivuma  akaomba adhabu kali.

Upande wa utetezi ukaiomba mahakama kutumia mwezi wa Kwarezima kuwapunguzia adhabu kwani wana umri mdogo miaka 28-29, wanategemewa na familia na watoto wao, hawana rekodi ya kutenda makosa mengine na mazingira ya kosa wote walikuwa wamelewa.

Jaji Mlacha akasema ulevi sio utetezi wa jinai yoyote lakini kutokana na mazingira ya kosa lilivyo tendeka  akawahukumu kwenda jela miaka miwili.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe