Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jela miaka 3, adai alifanya kosa sababu ya njaa

Jumapili , 6th Oct , 2019

Mahakama ya Wilaya ya Lindi, mkoani Mtwara, imemuhukumu mkazi wa Mitema aliyefahamika kwa jina la Kijazi Ally (29), kifungo cha miezi 36 jela baada ya kupatikana na hatia ya makosa mawili, likiwemo la kuvunja nyumba usiku na kuiba.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mshtakiwa aliulizwa kama anazo sababu za msingi, zitakazoishawishi Mahakama isimpe adhabu kali kwa makosa aliyokutwa nayo, ambapo katika kujitetea kwake alikiri kosa hilo na kudai kuwa ilikuwa ni mara yake ya kwanza na alilitenda kwa sababu ya njaa na kuahidi kutorudia tena.

Baada ya utetezi huo, Hakimu Kiswaga alimuuliza Mwanasheria wa Serikali Godfrey Mramba, kama ana kumbukumbu ya makosa ya zamani kwa mshtakiwa,ambapo alijibu kuwa hana lakini aliomba apewe adhabu kali, kwani ni mwizi mzoefu anayesumbua wakazi wa Mji wa Lindi.

Mramba alisema licha ya kutokuwa na kumbukumbu kwa makosa ya zamani kwa mshtakiwa,lakini tayari anakabiliwa na kesi nyingine inayohusu vitendo vya uvunjaji wa nyumba za watu nyakati za usiku na ipo katika Mahakama hiyo.

Kufuatia kesi  hiyo namba 14/2019, Hakimu Kiswaga alimhukumu mshtakiwa huyo kifungo cha miezi 36.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto