Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jeshi la Polisi lazungumza tishio la shambulio

Jumatano , 19th Jun , 2019

Kufuatia uwepo wa taarifa za  tishio la shambulio katika maeneo ya Masaki, hususani katika hoteli na migahawa, Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa amesema wanazo taarifa hizo na wanafuatilia.

Kamanda Lazaro Mambosasa

Akiongea na www.eatv.tv Kamanda Mambosasa, amesema taarifa hizo zipo, na wao kama jeshi la Polisi wanaendelea kufuatilia kwa karibu.

''Ni kweli taarifa zipo zinasambaa na sisi tunafuatilia, watu watulie tu kwasababu unaweza ukakuta mtu mmoja tu ameanzisha'', Mambosasa.

Aidha kabla ya kuongea na Mambosasa, www.eatv.tv ilimtafuta Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni, (ACP) Mussa Taibu ambaye aliweka wazi kuwa wamejipanga na kuimarisha usalama.

''Tumejipanga na vikosi vyetu kama kawaida kuhakikisha tunaimarisha usalama wetu na tunahakikisha maeneo yote yana usalama wa kutosha na sio wka hili tu, muda wote vikosi vyetu vipo tayari'', amesema Kamanda Taibu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ubalozi wa Marekani, maeneo yanayohofiwa huenda shambulio likafanyika ni Masaki katika hoteli na migahawa.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava