Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kauli ya Polepole kwa waliojinadi mitandaoni

Jumatatu , 13th Jul , 2020

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole, amewaonya wale wote waliokuwa wametengeneza vipeperushi na mabango na kuyaweka mitandaoni ya kwamba wanatangaza nia ya kugombea Ubunge katika jimbo fulani, waache mara moja kwa kuwa wameanza kampeni kabla ya wakati.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole.

Polepole ametoa kauli hiyo hii leo Julai 13, 2020, Jijini Dodoma, wakati akitoa ratiba ya mchakato mzima wa kuwapata wagombea wa nafasi za Ubunge na Uwakilishi kwa upande wa Zanzibar, ambapo amesema kuwa tayari amekwishaona watu wanavyosambaza mabango yao wakijinadi.

"Tumeshaanza kuona watu wanabandika mabango mitandaoni mnatangaza nia, ndugu yangu lile ni kosa, umeanza kampeni kabla ya wakati, kule ni kujipitisha kimtandao kwa wanachama, vipi yule ambaye hawezi kujitangaza kwa mtindo huo, ninawaonya muache mara moja kutumia mabango na vipeperushi kabla ya mchakato wa uchaguzi, fomu zitaanza kuchukuliwa kesho, wewe unaanza kujipiga mabango ni kinyume na taratibu tulizojiwekea" amesema Polepole.

 

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji