Vicky Kamata, akiwa na mume wake Dkt.Servacius Likwelile, wakati wa uhai wake
Vicky Kamata, ameyaandika hayo hii leo Februari 20, 2021, kupitia akunti yake ya mtandao wa Instagram.
"Nilidhani mimi ni jasiri, lakini kwa hili kumbe mimi si lolote, Mungu mbona umeniacha?", ameandika Vicky Kamata
Dkt. Servacius Beda Likwelile, amewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini ikiwemo kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na pia aliwahi kuwa Mhadhiri Idara ya Uchumi na Ndaki ya Sayansi ya Jamii Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.