Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kivuko kipya, watu zaidi ya 200, Ukara

Jumatatu , 24th Sep , 2018

Rais John Pombe Magufuli amemwagiza Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Isaack Kamwele kuitisha mapema iwezekanavyo zabuni ya ujenzi wa kivuko kipya ili wananchi wa Bugolora na Ukara wapate huduma nzuri baada ya kile cha MV Nyerere kuzama.

Kivuko cha Mv Nyerere kilichozama Septemba 20, 2018.

Hilo limebainishwa leo na Waziri mkuu Kassim Majaliwa, wakati akiongea kwenye eneo la tukio huko Ukara, Ukerewe, ambapo amesema pamoja na maamuzi ya kuvunja bodi ya TEMESA na kutengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya SUMATRA, lakini pia Rais Magufuli ameagiza ujenzi wa kivuko kipya, kitakachohudumia wakazi wa eneo la Ukara na Bugolora.

''Rais ameagiza leo Waziri aitishe zabuni ya ujenzi wa kivuko kipya chenye uwezo wa kubeba tani 50, na abiria zaidi ya 200 na itakuwa na uwezo mara mbili ya Mv Nyerere pia kiwe na uwezo wa kufanya safari nyingi ili kuepusha kuzidisha watu'', amesema.

Pia Waziri mkuu amemsisitiza waziri Kamwele ikiwezekana kufikia kesho awe ameshatangaza zabuni hiyo na ujenzi uanze mara moja ili wananchi wapate huduma ya haraka.

Aidha Waziri Majaliwa amemwagiza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo, kuhakikisha kivuko cha Mv Nyerere kinaondolewa majini vizuri na kisivutwe ili kuepusha uharibifu na hatimaye kiweze kuchunguzwa na kama kitawezekana kufanyiwa marekebisho kifanyiwe na kikikamilika kisaidiane na kivuko kipya.

Kivuko cha Mv Nyerere ambacho kilizama Alhamis ya Septemba 20, 2018, kilikuwa na uwezo wa kubeba tani 25 pamoja na abiria 100.  Katika ajali hiyo imebainika kivuko hicho kilizidisha idadi ya watu pamoja na mizigo.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa