Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Maambukizi ya Ukimwi yapungua kidogo sana 

Jumatano , 12th Mei , 2021

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Leonard Maboko amesema maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi yanakadiriwa kufikia watu 68,000 kwa sasa, tofauti na maambukizi ya utafiti uliofanywa mwaka 2016/2017 ambapo maambukizi mapya yalikuwa ni watu 72,000.

Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Leonard Maboko

Akizungumza katika mahojiano yake na Kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio, Dkt. Maboko amesema ipo haja ya tafiti kutilia mkazo takwimu za maambukizi mapya ya virusi hivyo ili kujua kama maambukizi yanapungua badala ya kuangalia takwimu za watu wanaoishi na Ukimwi kwani hazitosaidia.

"Maambukizi mapya ya Virusi ya Ukimwi bado yana hati hati japokuwa kuna hali ya kupungua, utafiti tuliofanya 2016/17 kwa mwaka ilkuwa watu 72,000 wamepata maambukizi mapya, sasa hivi kwa makadirio utafiti bado maambukizi mapya ni  watu 68000, kuna dalili za kupungua kwa maambukizi mapya ya Ukimwi ijapokuwa sio kwa kasi tuliyoitarajia," amesema Dkt. Maboko.

Akizungumzia maambukizi kwa upande wa vijana Dkt. Maboko amesema changamoto iliyopo ni kuongezeka kwa kasi ya maambukizi kwa vijana wa miaka 15- 24, huku akieleza kuwa vijana wakike wakiwa na silimia 80% katika maambukizi hayo.

"Changamoto ya maambukizi mapya ni vijana wa miaka 15 - 24 ndio wanaambukizwa zaidi kwa sasa hivi, kwa kila watu 10 wanaoambukizwa virusi 4 wanakuwa ni vijana, ukichukua vijana walioambukizwa 80% ya hao vijana ni wa kike, kwa lugha rahisi kila vijana 10 wanaopata maambukizi mapya 8 ni vijana wa kike na 2 ni wa kiume," amesema Dkt. Maboko.

Pia Dkt. Maboko amesisitiza vijana kuendelea kuchukua tahadhari za kutosha ili kukabiliana na maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ili kunusuru kizazi hicho kinachotegemewa na taifa kwa kuwa ni nguvu kazi.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA