Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Magufuli azindua ujenzi wa 'fly over' Tazara DSM

Jumamosi , 16th Apr , 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa barabara ya juu (Fly Over) kwenye makutano ya barabara za Mandela na Nyerere eneo la Tazara jijini Dar es salaam.

Ujenzi huo wa barabara hiyo ya juu unatarajia kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 100 ambapo inajengwa kwa ushirikiano wa serikali ya Japan na Tanzania ambapo Tanzania ikichangia Bilioni 8.36 na Japan Bilioni 93.44.

Akizungumza katika shughuli hiyo Rais Dkt. Magufuli amewataka raia watakao ajiriwa katika mradi huo wawe waaminifu na kujiepusha na wizi wa mafuta kufanya migomo au wizi wa vifaa vya ujenzi.

Rais pia ametoa shukrani kwa serikali ya Japan kwa kuendelea kuisaidia Tanzania bila kuweka masharti magumu kama walivyo baadhi ya wafadhili.

''Ni bora kula muhogo wa kujitafutia mwenyewe kuliko kula mkate wa masimango'' Amesema Rais Magufuli.

Aidha akitoa salamu za Mkoa wa Dar es salaam Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amemuhakikishia Rais Magufuli kwamba viongozi ambao wapo chini yake wapo tayari kumuunga mkono katika jitihada za kuleta maendeleo ya taifa.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava