Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mapambano dhidi ya ujangili kuendelea - Serikali

Alhamisi , 8th Dec , 2022

Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imesema itaendelea kuongeza nguvu katika jitihada za Kuzuia na Kupambana na ujangili wa wanyamapori na Biashara ya nyara na mazao ya misitu ili kutokomeza kabisa vitendo hivyo vinavyoathiri taswira ya nchi, uchumi na maendeleo ya uhifadhi

Hayo yamebainishwa leo jijini Arusha wakati wa ufunguzi wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wenyeviti wa Kamati za Kanda za Kiikolojia za Kuratibu Doria (TCG's) katika kukabiliana na ujangili na Biashara haramu ya wanyamapori nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Msaidizi wa Uzuiaji Ujangili na Mwenyekiti wa Kikosi Kazi Taifa cha Kuzuia na Kupambana na Ujangili nchini Bw. Robert Mande , Afisa Wanyamapori Mkuu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. John Ngowi amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mafunzo na doria ili kuhakikisha majangili wanaokamatwa wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Amesema mkakati uliopo katika mapambano dhidi ya ujangili ni kuona watuhumiwa wote wanaokamatwa wanafikishwa mahakamani na mashauri yao yanaendeshwa haraka na kwa ufanisi ili adhabu inayostahili iweze kutolewa kulingana na matakwa ya sheria.

“Lengo la kutolewa kwa mafunzo haya ni kuharakisha na kuhakikisha majangili wote wanaokamatwa wanafikishwa mahakamani na mashauri yao yanaendeshwa kwa haraka na kwa ufanisi ili wahusika wapewe adhabu inayostahili kulingana na matakwa ya sheria za nchi yetu” Amesisitiza.

Amesema ujangili unaathiri ustawi wa jamii na kudumaza uchumi wa nchi hivyo  mafunzo hayo yatawasaidia Wenyeviti hao kupanga mikakati endelevu ya kukabiliana na ujangili huku akibainisha kuwa mitandao ya uhalifu wa rasilimali hizo wakati mwingine huanzia nje ya nchi ikihusisha watu wengi katika ngazi mbalimbali na inafadhiliwa na watu wenye uwezo mkubwa wa kifedha.

'' Ni imani yangu kuwa baada ya mafunzo haya wananchi wataanza kuona majangili wanachukuliwa hatua kali za kisheria zinazostahili.  Wataanza kuogopa kushiriki katika  vitendo vya ujangili'' Amesema Afisa Wanyamapori Mkuu, Ngowi

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yatasaidia Watendaji wa Idara na Taasisi zinazohusika na ulinzi na uhifadhi wa wanyamapori na mazao ya misitu kupanga mikakati endelevu ya kukabiliana na ujangili hapa nchini pamoja na kuimarisha dhana ya umoja inayowezesha Idara na Taasisi za ulinzi wa wanyamapori na misitu kufanya kazi kwa pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Kupambana na Ujangili na Usafirshaji haramu wa Nyara, Theotimos Rwegasira amesema mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo Duniani (UNDP) na Shirika la Mazingira (GEF) yatasaidia kupunguza ujangili kwa kiwango kikubwa.

 Amesema mafunzo hayo yatakayohitimishwa leo yanatarajiwa kuleta mafanikio makubwa katika vita dhidi ya ujangili ikiwa ni mwendelezo kuunga juhudi mkono juhudi za serikali za kukabiliana na ujangili.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava