Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Matokeo ya kidato cha pili, darasa la nne kufutwa

Jumatatu , 12th Nov , 2018

Baraza la mtihani la taifa (NECTA), limesema kuwa halitosita kuvifuta vituo ambavyo vitahatarisha usalama wa mitihani ya taifa inayoendelea nchini kwa kidato cha pili na darasa la nne, pamoja na kufuta matokeo ya watahiniwa.

Katibu mtendaji wa NECTA, Dkt. Charles Msonde.

Hayo yamebainishwa na Katibu mtendaji wa NECTA, Dkt. Charles Msonde ambapo amesema kuwa, watakaohusika na kukiukwa kwa kanuni za mitihani watawajibishwa kwa mujibu wa sheria zilizopo.

"Watahiniwa watambue kuwa kukiuka kanuni za upimaji au kufanya udanganyifu kutafanya wafutiwe matokeo yao yote, lakini pia Baraza halitosita kukifuta kituo chochote cha mtihani endapo litajiridhisha kuwa uwepo wake unahatarisha usalama wa upimaji wa taifa", amesema Dkt. Msonde.

Wanafunzi wa kidato cha pili wameanza mitihani yao leo Novemba 12, kote nchini na watamaliza Novemba 23, huku wanafunzi wa darasa la nne wao wataanza tarehe 22 na 23 mwezi huu.

Hayo yanajiri ikiwa ni miezi michache tu tangu Baraza hilo lilipofuta matokeo ya darasa la saba kwa baadhi ya shule nchini kutokana na udanganyifu, ambapo shule zilizofutiwa ni, shule za msingi zote zilizopo ndani ya Halmashauri ya Chemba, pamoja na baadhi ya shule katika halmashauri ya Kondoa, Kinondoni, Mwanza jiji na Ubungo kwa kosa la kuhusika kwa kuvujisha kwa mitihani ya darasa la saba ikiwa ni kinyume na taratibu na kanuni za mitihani nchini.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine