Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mawaziri waliotumbuliwa walivyowabana Mawaziri

Jumamosi , 17th Nov , 2018

Siku chache baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, kutengua uteuzi wa waliokuwa mawaziri wa Viwanda na Uwekezaji Charles Mwijage pamoja na aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Charles Mwijage wawili hao waliibuka bungeni wiki hii.

Waliokuwa Mawaziri Charles Mwijage na Charles Tizeba.

Wawili hao ambao walikuwa watu wa karibu kupitia taasisi za wizara zao, waliuliza maswali bungeni kwa nyakati tofauti maswali ambayo yalikuwa wakiuliza  kwa waliolkuwa wajumbe wenzao kwenye baraza la Mawaziri lakini wao wakiwa kama wabunge wa majimbo yao husika.

Novemba 13 aliyekuwa Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba, alihudhuria vikao vya Bunge jijini Dodoma na kushangiliwa na Wabunge, pale Naibu Spika Tulia Ackson alipomtaja ili kuuliza swali la nyongeza kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Dkt. Tizeba ambaye pia ni Mbunge wa Buchosa, alisimama na kupigiwa makofi na wabunge wenzake, kisha akamuomba Naibu Spika kumruhusu kusema maneno mawili tu, na kusema kwamba.

La kwanza ni kumshukuru sana Mh. Rais Magufuli kwa Fursa aliyokuwa amenipa ya kulitumikia taifa, lakini pia nikushukuru wewe na Mheshimiwa Spika kwa ushirikiano nilioupata wakati nikitumika serikalini ndani ya Bunge lako”.

Kauli hiyo iliendelea kupigiwa makofi na Wabunge wenzake, na kisha akauliza swali alilokusudia, ambalo lilihusu ujenzi wa vivuko vilivyomo kwenye jimbo lake la Buchosa.

Novemba 16 aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage ameibuka na kuzungumza bungeni, kwa mara ya kwanza tangu atenguliwe nafasi yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli wiki iliyopita.

Akizungumza Bungeni Jijini Dodoma kabla hajauliza swali kwa Wizara ya Nishati, Mwijage amelishukuru bunge hilo kupitia kwa Spika Job Ndugai wakati wote wa Uwaziri wake ndani ya Bunge.

Nawashukru sana tangu mlivyokuwa mkiniongoza bungeni, kupitia kwako Mwenyekiti napenda kumshukuru Rais,  Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kwa namna ambavyo waliniamini na kunisimamia kwenye majukumu ambayo walinipa.”

Wiki iliyopita, Rais Magufuli alipokuwa akiwaapisha mawaziri wapya wawili na naibu mawaziri wanne, alibainisha kuwa Charles Mwijage, na Charles Tizeba walishindwa kufanya maamuzi wakati wafanyabiashara wa korosho waliposhindwa kununua korosho za wakulima.

"Nilimwambia Waziri Mkuu awakumbushe mawaziri wake, kwa sababu matatizo mengi yaliyokuwa yakihusu kilimo na viwanda yalikua yanamalizwa na Waziri Mkuu, nilijiuliza pia kahawa ni kilimo pia vipi Waziri hakuliona pia." Rais Magufuli.

"Nilijiuliza kwanini hawa tuliowapa, majukumu hawafanyi hivi, ni ukweli pia bei ya soko la korosho limeshuka kidogo unapoona kuna tatizo unamtuma Waziri Mkuu anatatua," aliongeza Rais Magufuli.

HABARI ZAIDI

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji