Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mchujo CCM, wajumbe kazini leo

Alhamisi , 30th Jul , 2020

Mchakato wa mchujo kwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walioomba kugombea Udiwani, unaanza leo kwa vikao vya chama hicho vya Kata kuwajadili wagombea. 

Bendera za CCM

Kwa upande wa wagombea Ubunge na uwakilishi kwa Zanzibar, vikao vya majimbo pia vinaanza leo, huku vikao vya Wilaya kwa upande wa Tanzania Bara, vinatarajiwa kuanza keshokutwa hadi Agosti 2, mwaka huu.

Tayari CCM imekamilisha mchakato wa kura za maoni kwa ngazi ya Ubunge, Udiwani na uwakilishi, ulioanza tangu Julai 14 na kukamilika Julai 17, mwaka huu, kwa mara ya kwanza katika historia ya CCM, kulikuwa na idadi kubwa ya wanachama waliojitokeza kuchukua fomu, kuomba kuteuliwa kugombea nafasi hizo, kwa ngazi ya Ubunge pekee, jimbo moja idadi ya chini ya wanachama waliojitokeza ilikuwa si chini ya watu 30.

Dar es Salaam kuna Wilaya tano na majimbo 10, ambapo Wilaya ya Ubungo ina majimbo ya Ubungo na Kibamba, Wilaya ya Kinondoni ina majimbo ya Kinondoni na Kawe na wilaya ya Temeke ina majimbo ya Mbagala na Temeke.

Aidha, wilaya ya Ilala ina majimbo ya Ilala, Segerea na Ukonga na Wilaya ya Kigamboni ina jimbo moja la Kigamboni. 

Baada ya vikao vya Kata kujadili wagombea wa udiwani, vitatoa mapendekezo kwa kamati za siasa za wilaya, ambazo zitatoa mapendekezo kwa Halmashauri Kuu za Mikoa ambazo zitajadili wagombea na kuteua wagombea wa udiwani mmoja katika kila kata mkoani humo. 

Kwa upande wa Ubunge, baada ya vikao vya wilaya kupendekeza majina ya wagombea watakaokiwakilisha chama hicho kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba 28, mwaka huu, maoni ya vikao hivyo yatawasilishwa kwa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM. 

Kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt John Magufuli itateua jina moja la mwana CCM ,atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi wa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA