Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkurugenzi Chato lawamani kudorora uandikishaji

Jumanne , 25th Nov , 2014

Viongozi wa vyama vya siasa Wilayani Chato mkoa wa Geita, wamemlalamikia mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw. Clement Berege kuwa ndiye chanzo cha kusuasua kwa uandikisha wa Wananchi uchaguzi wa Serikali za Mitaa wilayani humo.

Mkurugenzi wa halmashauri ya Chato Bw. Clement Berege.

Akizungumza na Ea Radio, katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) wilayani humo, Khamis Mkaruka, amesema lawama za kudorora kwa zoezi hilo zinamwangukia mkurugenzi huyo kwa kushindwa kutoa matangazo mbalimbali ya kuwahamasisha wananchi wenye sifa kujitokeza kwa wingi ili kujiandikisha.

Mkaruka amesema kama kiongozi wa chama, ametimiza wajibu kwa kuwahamasisha wanachama na mashabiki wa chama chake kwenda kujiandikisha, lakini wanakwamishwa na mkurugenzi Berege.

Kwa upande wake, katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Chato, Mange Ludomya, amesema inawashangaza kuona mkurugenzi anawapuuza wananchi kujiandikisha katika daftari la kupigia kura, hatua inayoweza kusababisha wengi kukosa haki yao ya msingi ya kuwachagua viongozi wanaowataka.

Hata hivyo, mkurugenzi huyo alipotafutwa na Ea Radio, hakuweza kupatikana ili kutolea ufafanuzi lawama hizo za vyama vya siasa.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu