Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mtoto aliyetekwa miezi 7 arudi mwenyewe

Jumamosi , 13th Apr , 2019

Mtoto Idrissa Ally (13), mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Pronces Gate jijini Dar es Salaam, amerejea nyumbani kwa wazazi wake baada ya kutekwa na watu wasiojulikana Septemba 26, 2018.

Idrissa alirejea nyumbani jana April 12 majira ya jioni, huku wazazi wake ambao walikuwa tayari wamekata tamaa, walimpokea na kujawa na furaha iliyotoweka kwa kipindi kirefu.

Tangu Septemba 2018 siku alipotekwa hadi April 2019 (jana) alipopatikana, Idrissa amefikisha siku 198 za kuishi mbali na familia yake huku akishindwa kuendelea na masomo.

Baba mzazi wa Idrissa amesema jana jioni, mama mzazi wa mtoto huyo, Leila Kombe, alipokea ujumbe kutoka katika namba asiyoifahamu na kuelezwa kuhusu kutafutwa na mtoto wake. Hata hivyo, hakuamini kwa kuwa ameshapokea ujumbe wa aina hiyo mara nyingi, kumtaka mume wake apige namba hiyo.

"Nilimpigia akaniambia yupo Ubungo na kwamba mtoto wake aliomba ampigie lakini ameshaondoka akielekea nyumbani kwao Tegeta”, amesema Idd ambaye ni baba wa kijana huyo.

Amesema hakuamini lakini kama miujiza saa moja jioni aliona pikipiki ikiingia nyumbani kwake ikiwa imempakia kijana wake, “bado siamini kama amerudi nyumbani, tumekuwa kwenye giza nene kwa muda mrefu", amesema  Baba wa mtoto huyo.

Mzazi wa mtoto huyo amesema mwanaye amebadilika na kuwa mrefu, huku akiwa na nywele nyingi, “inaonekana hakuwahi kunyoa tangu alipotekwa”.

Akiendelea kuhojiwa ni kwa namna gani ameweza kuachiwa alikotekwa, Idrissa amesema kuwa kuna kijana mmoja alimsaidia kumtorosha, alimpatia nauli akimtaka aende Dar es Salaam kwa wazazi wake.

Idrissa alitekwa Septemba 26,2018 saa 11 jioni akiwa anacheza na wenzake eneo la Tegeta Masaiti wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam, ambapo alichukuliwa na dereva mwanaume aliyekuwa katika gari aina ya Toyota IST. Dereva huyo alitoa kichupa kidogo kinachodhaniwa ni ‘spray’ na kumpulizia mtoto huyo na kumuingiza mlango wa nyuma wa gari na kuondoka naye.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava