Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwanamke apambana na jambazi kumwokoa mumewe

Jumapili , 9th Dec , 2018

Mwanamke mmoja mkazi wa Kijiji cha Mahyolo, wilayani Bunda mkoani Mara, Busimba Malegesi, ameonyesha ushujaa wa aina yake baada ya kumwokoa mume wake baada ya kuvamiwa na jambazi mwenye silaha ambaye aliwaingilia usiku nyumbani kwao wakiwa wamelala.

Waziri Lugola alipofika hospitali kumjulia hali, Samson Malegesi aliyekatwa na mapanga baada ya kuvamiwa nyumbani kwake.

Mtu huyo alivamia nyumba hiyo kwa kuvunja mlango, na kuanza kumshambulia mume wa Busimba, Samson Malegesi (62) kwa kumkatakata mapanga mwili mzima.

Busimba alipoona hali hiyo, alimrukia jambazi huyo kiunoni na kumwangusha chini na kumnyang’anya panga pamoja na tochi ambayo alikuwa nayo wakati anamshambulia mumewe.

 “Baada ya kuingia aliwasha tochi na kuanza kumsaka Malegesi, alipomwona alianza kumshambulia kwa kumcharanga mapanga kichwani, mikononi, kwenye mbavu na kusababisha damu nyingi kumwagika", amesimulia mwanamke huyo.

Ameongeza kuwa, "Wakati jambazi huyo akiendelea kumshambulia mume wangu, nilianza kupambana naye ili kumnusuru mume wangu na hatimaye jambazi nilimzidi nguvu kwa kumuangusha chini".

Akiwa katika ziara yake ya kikazi mjini Bunda, Waziri Lugola alimpongeza mwanamke huyo na kumuelezea kuwa ni shujaa kwa kitendo alichokifanya.

Nampongeza sana mwanamke aliyepambana na jambazi na kufanikiwa kumwokoa mume wake. Hakika kama si ushujaa wa mwanamke huyo, mume wake tungempoteza kwa sababu jambazi huyo alidhamiria kumuua kwa kumkata mapanga zile sehemu ambazo ni hatari zaidi kwa uhai wa ubinadamu", amesema Lugola.

"(Mkuu wa Kituo cha Polisi) hakikisheni hamlali mpaka mnalipata hili jambazi kwa kutumia njia zote za kiintelejinsia mlizosomea ili kumkamata haraka iwezekanavyo", ameongeza Lugola.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA