Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

NCCR Mageuzi yadai kuvuna wanachama elfu 90

Alhamisi , 21st Mei , 2020

Chama cha NCCR Mageuzi kimewapokea wanachama takribani 90,000 kutoka vyama mbalimbali vya siasa katika mikoa ya Shinyanga na Mara, akiwemo aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga, ambao wamevihama vyama vyao.

Wanachama wapywa wa NCCR Mageuzi mkoani Shinyanga

Akizungumza na wanahabari Mjini Shinyanga baada ya kupokea wanachama wapya zaidi ya 12,000 kutoka Jimbo la Shinyanga, Mkuu wa Idara ya Uenezi wa NCCR Mageuzi nchini, Edward Simbeye amesema kuwa mkoa wa Mara una wanachama 48,000 na mkoa wa Shinyanga ukiwa na wanachama 42,000.

"Ukijumlisha kwa mikoa hii miwili tu, tuna wanachama 90,000, mkoa wa Mara tuna wanachama 48,000 na mkoa wa Shinyanga kwa mujibu wa mwakilishi wetu aliyekuwa akiendesha zoezi hili, tuna wanachama 42,000", amesema Simbeye.

Naye aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga, Shigano Charles Mapema akitangaza kukihama chama hicho pamoja na mwenzake aliyewahi kuhudumu kitengo cha Operesheni ya Chadema ni Msingi, Majimbo ya Solwa, Kongwa na Temeke, Yunis Kanumba wamesema kuwa hawajaridhishwa na jinsi CHADEMA inavyowafanyia baadhi ya wabunge wake.

Baadaye Mkuu wa Idara ya Uenezi wa NCCR Mageuzi nchini, Edward Simbeye akaweka wazi msimamo wa chama chake kuwa kimejipanga kusimamisha mgombea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava