Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

NEC yatolea ufafanuzi vituo vya upigaji kura

Alhamisi , 8th Oct , 2015

Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC imetolea ufafanuzi kuhusu vituo vya kuandikisha kupiga kura, karatasi za kupigia kura na utaratibu wa upigaji wa kura huku wakiwataka viongozi wa vyama vya siasa kuwaambia ukweli wananchi na kufuata sheria za Uchaguzi

Mkurugenzi wa masuala ya Sheria wa NEC, Bw Emmanuel Kawishe

Akiongea na East Africa radio Mkurugenzi wa masuala ya Sheria wa NEC, Bw Emmanuel Kawishe amesema kuwa ugawaji wa vituo vya kupigia kura umefuata sheria na vituo vimegawanywa kwa vipengele ili kurahisisha upigaji kura kwa wananchi na hakuna kituo chochote kilichoongezeka.

Aidha Bw, Kawishe ameongeza kuwa viongozi waache kuwadanganya wananchi kuhusu karatasi za kupigia kura kuwa zinahamisha alama za mgombea na kusema kabla ya kupeleka vituoni vyama vyote vinahakiki karatasi hizo huku akiwataka wananchi kufuata sheria ya kutokuweka mikusanyiko mara ya kupiga kura kama wanavyoelekezwa na viongozi wa vyama vyao.

Kawishe amesema kuwa kwa mujibu wa sheria kila chama kinatakiwa kuweka wakala ndani ya chumba cha upigaji kura na ndio mwenye jukumu la kuhesabu kura, hivyo kuweka mikusanyiko isiyokuwa na kibali ni kuhatarisha amani kwa kuwa ni kinyume cha sheria.

Amesema tume inaendesha mchakato wa uchaguzi mkuu kwa mujibu wa sheria kama ilivyofanya miaka ya nyuma na itatangaza matokeo kwa utaratibu ule ule ambao utaondoka kero na sintofahamu kwa vyama na wananchi kwa ujumla.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine