Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Niliogopa kumuuliza Mwinyi eneo la kumzikia" -JPM

Jumatano , 29th Jul , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, amesema kuwa Serikali ilikwishatenga eneo maalum la maziko kwa viongozi wakuu wa Kiserikali watakaofariki, ambapo watazikwa Dodoma, kwa kuwa ndiko yaliko Makao Makuu ya Nchi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli, akiwa na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Julai 29, 2020, wakati wa shughuli ya mwisho ya mazishi ya Rais Mstaafu Hayati Benjamin Mkapa, ambapo amesema kuwa miaka kadhaa iliyopita Rais Mkapa kabla ya kufariki, alimfuata na kumuomba endapo ataaga Dunia, basi ataomba azikwe kijijini kwao Lupaso, ambapo aliogopa kumuuliza Mzee Mwinyi eneo atakalozikiwa kwa kuwa umri wake ulikuwa ni mkubwa zaidi.

"Kuna wakati Serikali ilipanga mahali pa maziko kwa viongozi na tulipangiwa kuwa tunazikwa Dodoma, Mzee Mkapa akaniuliza mlipanga maziko yawe Dodoma, mimi msinizike Dodoma nikasema wewe unataka wakuzike wapi akasema Lupaso, Mzee Kikwete akasema Msoga, nikaogopa kumuuliza Mzee Mwinyi kwa sababu alikuwa na miaka zaidi ya 90 na mimi nilisema nitazikwa Chato" amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli ameongeza kuwa, "Mkapa alipenda kwao, kwenye hili Watanzania tujifunze, Mzee Mkapa angeweza kuzikwa Dar es Salaam au Lushoto, lakini ndani ya dhamira yake alitaka azikwe mahali alipozaliwa katika kijiji cha Lupaso, najua Maaskofu mnaniangalia sana kwa sababu ninyi huwa mnazikwa kwenye makanisa". 

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto