Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Nitakwenda kuwajua hukohuko CCM"- Pauline Gekul

Jumapili , 14th Oct , 2018

Baada ya aliyekuwa Mbunge wa Babati Mjini (CHADEMA), Pauline Gekul kutangaza kujiuzulu wadhifa huo na kujiunga na CCM , amesema kuwa matabaka na kudharaulika ndani ya chama ndiyo sababu iliyopelekea yeye kukihama chama hicho huku akikiri kuwa hakifahamu vizuri chama hicho licha ya kuhamia.

Aliyekuwa Mbunge wa Babati Mjini (CHADEMA), Pauline Gekul.

Akizungumza na www.eatv.tv, Gekul ameeleza kuwa amefanya hivyo ili kutimiza wajibu kwa wananchi wake kwani anashindwa kuzitimiza ahadi hizo akiwa upande wa upinzani.

Gekul amezungumzia suala la kuwa huenda amelipwa pesa ili kujiunga na CCM, ambapo amesema kuwa "Sijanunuliwa na nina kwenda CCM nikiwa siwafahamu kabisa lakini nashukuru nimepata mapokezi mazuri na nitakwenda kuwajua huko huko, wala sijanunuliwa kama wanavyosema".

Gekul amesema kuwa amechoshwa na matabaka yaliyomo ndani ya CHADEMA, kutokusikilizwa na kuthaminiwa kwa baadhi ya watu na wengine akidai kuwa wanaonekana kama chaguo la tatu mbele ya viongozi.

Barua ya kujizulu kwa Gekul ilianza kusambaa kwa kasi mitandaoni jana, Oktoba 13, saa 4 usiku kwenda kwa Spika wa Bunge Job Ndugai, ambapo sasa anaungana na wengine waliojizulu hivi karibuni akiwemo, Mwarya Chacha (Serengeti) na James Milly wa Simanjiro, wote wa CHADEMA.

Gekul anakuwa Mbunge wa nane kujiuzulu kutoka upinzani kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) na kupewa nafasi ya kugombea tena nafasi hiyo, wabunge hao ni; Dkt. Godwin Mollel (Siha-CHADEMA) na Maulid Mtulia (Kinondoni-CUF) huku wanaosubiri kuapishwa ni, Mwita Waitara (Ukonga), Julius Kalanga (Monduli) na Zuberi Kuchauka (Liwale-CUF) ambaye aliibuka mshindi katika uchaguzi uliofanyika jana Jumamosi Oktoba 13,2018 kwa ushindi wa asilimia 85.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava