Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ole Medeye 'ajitumbua mwenyewe' UDP

Jumatatu , 29th Mei , 2017

Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha 'The United Democratic Party' (UDP) ametangaza rasmi kujiuzulu nafasi hiyo kwa madai ya kujipa fursa ya kuitumikia familia yake.

John Cheyo (Kushoto) akiwa na Goodluck Ole Medeye

Ole Medeye ambaye alijiunga na UDP akitokea CHADEMA mapema mwaka jana, ametoa kauli hiyo leo katika barua aliyomuandikia Mwenyekiti wa chama hicho Mh. John Cheyo, huku akimshukuru kwa kumuani katika nafasi hiyo kwa kipindi chote.

"Napenda kukujulisha rasmi kwamba ili nipate muda wa kutosha kufanya shughuli za ustawi na maendeleo ya familia na jamii inayonitegemea nimeamua kwa hiari yangu kujiuzulu nafasi hiyo ya Katibu Mkuu kuanzia tarehe ya barua hii".Imesema sehemu ya barua hiyo

Mwanasiasa huyo amewahi kushika nyazifa mbalimbali ikiwemo Ubunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi kupitia CCM katika Bunge la 10 na kupitia nafasi hiyo aliweza pia kuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika serikali ya awamu ya nne.

Mara baada ya kushindwa katika kinyang'anyiro cha ubunge wa jimbo hilo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, aliamua kuhama chama na kujiunga na CHADEMA ambapo hakudumu sana licha ya CHADEMA kumpa nafasi ya kugombea nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kisha alihamia UDP kabla ya kupewa nafasi ya Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava