Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polepole ajibu kuhusu kuwasema wanaohama

Jumatano , 22nd Nov , 2017

Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Humphrey Polepole, amesema chama hicho kwasasa kimeweka misingi ambayo inawabana viongozi wasiotosheka lakini hakina tabia ya kuwasema vibaya wanachama wake wakihama.

Akiongea kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari Ndg. Polepole amesema kuwa Chama chao kinalinda misingi na Itikadi zake ambazo ni kuheshimu utu wa mtu pamoja na kuwatumikia raia hivyo kwa kiongozi ambaye hawezi kufanya hayo lazima atakimbia.

"Mimi kama Katibu wa Itikadi na Uenezi sijawahi kutoa tamko la kumsema vibaya mwanachama anayehama chama chetu kwasababu sio misingi na Itikadi zetu". Pia ameongeza kuwa ni dhambi kubwa kumhukumu mtu anapohama chama kimoja kwenda kingine.

“Hatuna tabia ya kuwasema vibaya wale wanaokihama chama, lakini tumegundua kwamba raia wa kawaida ndio wamekuwa na tabia ya kuwasema kwa sababu wanayaona matendo yao ya kutotosheka”, amesema Polepole.

Aidha Polepole amesisitiza kuwa CCM kwasasa imeweka misingi migumu itakayowabana wasiotosheka na wasio na kiasi ndio maana tumeamua kuweka sheria ya mtu mmoja, cheo kimoja. Sheria ambayo itawabana wenye kutaka vyeo vingi kwa wakati mmoja.

HABARI ZAIDI

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine