Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polisi Dar yaanzisha msako wa bodaboda

Jumanne , 11th Dec , 2018

Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es salaam limetangaza operesheni ya kuwakamata baadhi ya watumiaji wa vyombo vya usafiri ikiwemo bodaboda kwa kosa la kutumia barabara ya magari yaendayo haraka ikiwa ni siku chache baada ya kutokea kwa vifo vya raia wawili ambao waligongwa

Baadhi ya Madereva bodaboda

 gari ya mwendokasi.

Kauli hiyo ya Jeshi la Polisi imetolewa leo jijini Dar es salaam na Kamanda Lazaro Mambosasa ikiwa ni siku tatu zimepita tangu kutokea kwa ajali hiyo ambapo dereva wa bodaboda aliligonga basi hilo na kusababisha ajali iliyopelekea vifo vya abiria wawili eneo la Manzese Tiptop.

"Tunawashikiria madereva 20 kwa kuharibu basi la mwendokasi kwenye tukio lililotokea disemba 8 mwaka huu, niendelee kutoa onyo kwa madereva wa bodaboda kuhusu suala la matumizi ya barabara isiyokuwa kihalali," amesema Kamanda Mambosasa.

"Huyu dereva amejitakia kifo, kitendo cha kuingia kwenye barabara ya mwendokasi ni kujihatarisha maisha yake mwenyewe, kila mmoja aheshimu sheria za nchi na kila mmoja afuate taratibu za nchi na kwa jinsi tulivyojipanga hatutamuacha yeyote akivunja sheria," ameongeza Mambosasa.

"Yeyote ambaye ataendelea kupima nguvu yetu Kanda Maalum ya Dar es salaam haipimwi, bali ataishia kwenye mikono ya dola kama walivyo wahalifu wengine".

Pikipiki iliyopelekea kutokea kwa ajali hiyo imesajiliwa kwa namba T- 155 DCW ambapo baada ya tukio hilo baadhi ya madereva wa bodaboda waliokuwa kwenye eneo la ajali walianza kulishambulia gari la mwendo kasi na kusababisha uharibifu wa kioo cha mbele.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava