Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Polisi Kagera waua mmoja anayedhaniwa ni jambazi

Ijumaa , 9th Dec , 2022

Mtu mmoja anayedhaniwa kuwa ni jambazi amepoteza maisha baada ya kupigwa risasi na askari polisi, wakati yeye na wenzake wawili wakijiandaa kufanya uhalifu katika kituo cha mafuta cha Benaco Oil, katika kijiji cha Rwakalemera kata ya Kasuro tarafa Nyamiaga wilaya ya Ngara, mkoa wa Kagera.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera William Mwampaghale amesema kuwa Desemba 07 mwaka huu askari polisi wakiwa katika doria walipata taarifa fiche kuwa kuna watu wanajiandaa kufanya uhalifu wa kutumia silaha katika kituo hicho cha mafuta, na kuweka mtego wa kuwanasa.

Kamanda huyo amesema kuwa ilipofika saa 5:30 usiku, askari polisi wakiwa katika maficho waliwaona watu watatu na kuwaamrisha wasimame na kwamba baada ya watu hao kugundua kuwa wanasimamishwa na askari walianza kurusha risasi ovyo kuelekea walipokuwa askari, hali iliyosababisha askari hao kujibu na kumjeruhi mtu huyo aliyepoteza maisha wakati akiwahishwa hospitali.

"Askari hao walifanikiwa kumjeruhi mmoja, mmoja alitoroka na mwingine alijisalimisha, tulifanya upekuzi na kupata bunduki moja aina ya AK 47 na magazine tatu zikiwa na jumla ya risasi 25, aliyejisalimisha tunaendelea kumhoji ili kupata taarifa zaidi juu ya aliyetoroka lakini pia kujua wengine wanaoshirikiana nao kufanya uhalifu" amesema Mwampaghale.

Kuuawa kwa mtu huyo kumetokea ikiwa imepita wiki moja baada ya watu wengine watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kuuawa na polisi baada ya kutokea majibizano ya risasi katika eneo la Nyabugombe kata Nyakahura wilayani Biharamulo, Desemba 01 mwaka huu saa 8 usiku.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa