Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shanna
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shanna amesema kwa ushirikiano na maafisa wa TANAPA wa wilaya ya Serengeti, pamoja na askari wa mikoa ya kanda ya ziwa ikiwemo Mwanza, kigoma, Shinyanga, Simiyu na Mara waliweza kuwakamata watuhumiwa hao.
Shanna amesema Operesheni maalum ilifanywa na askari wa mikoa hiyo ilichukua takribani masaa 48 na kufanikiwa kuwabaini watuhumiwa hao pamoja na vifaa wanavyotumia kutemgenezea noti bandia
Aidha Kamanda Shana amewatahadharisha wananchi wa Mkoa wa Mwanza kuwa makini na fedha za watuhumiwa hao ambazo tayari zipo kwenye mzunguko.
Jeshi la polisi linaendendelea na mahojiano na watuhumiwa hao watano na uchunguzi utakapokamilika watafikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazowakabili, huku msako wa kuwatafuta watuhumiwa wengine waliotoroka bado unaendelea katika maeneo yote ya jiji la Mwanza na mikoa ya jirani.