Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais atoa neno kuhusu Kibiti, Rufiji

Jumanne , 20th Jun , 2017

Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amewaonya wanaojihusisha na vitendo vya mauaji wilayani Kibiti na Rufiji, mkoani Pwani, huku akisema kuwa vitendo hivyo ndivyo vinafanya maeneo hayo kukosa kiwanda hata kimoja.

Ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Pwani Mhe. Magufuli amesema kwamba watu wanaochelewesha maendeleo ya Wilaya ya Kibiti na Rufiji ni wananchi wenyewe ambao wanawaficha watu wanaofanya uhalifu ilhali wanaishi mitaani kwao.

"Tunaochelewesha maendeleo ya Kibiti na Rufifi ni sisi wenyewe, kwa sababu tunawaficha watu wanaofanya vitendo vya kihalifu na mauaji, tuna kaa nao na tunawajua huku wengine wakiwa ni watoto wetu, tumewaficha kwa hivyo mtaendelea kukaa bila kiwanda hata kimoja. Lakini niseme watanyooka na salamu ziwasifikie. Serikali ya awamu ya tano siyo ya kuchezewa na watanyooka hata hivyo wameshaanza kunyooka. Hawatapita na nimesema hawapiti", alisema Rais Magufuli.

Aidha pamoja na hayo Rais Magufuli  amesema atahakikisha anazitatua changamoto zinazosababishwa na viongozi ambao wana tamaa na wanatumia vibaya rasilimali za nchi kwa kuwachukulia hatua viongozi wazembe wanaorudisha maendeleo nyuma.

“Niwahakikishie ndugu zangu kuwa nitalala nao mbele kwa nguvu zangu zote. Nitalala nao mbele kwa kumtanguliza Mungu ili maisha ya Watanzania yabadilike” Mhe. Magufuli aliongeza.

 

 

 

 

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava