Rais wa Zambia Hakainde Hichilema
Rais Hichilema amesafiri kwenda kwenye Mkutano wa Umoja wa Mataifa kwa kutumia ndege ya shirika la ndege la Qatar akitokea uwanja wa ndege wa Lusaka akiambatana na mawaziri wawili tu.
Rais Hichilema ambaya amekuwa akisisitiza matumizi mazuri ya rasilimali za nchi, amesafiri na Waziri wa Mambo ya Nje Stanley Kakubo na Waziri wa Fedha Dk. Situmbeko Musokotwane.
Kwa kitendo hicho Rais Hichilema amepongezwa mitandaoni kwa kubana matumzi ya serikali huku wakitolewa mifano ya mataifa ya Zimbabwe na Malawi kwa kusafiri maafisa wengi safari za nje