Rais Magufuli na Katibu Mkuu wa CCM Bashiru Ally
Akiongea leo Jijini Dar es Salaam baada ya kuzindua jengo la Jitegemee linalomilikiwa na chama hicho ambalo limefanyiwa ukarabati, amesema hayo ni matokeo ya jitihada za Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru.
''Ufisadi ulikuwa umeshamiri, mali za chama zilikuwa zimeshaanza kuchukuliwa na watu binafsi lakini nilipomteua Dkt. Bashiru kuwa Katibu Mkuu na akaanza kuzifuatilia watu wakasema ni CUF na mimi nikasema nataka CUF wa namna hii ndani ya CCM,'' alisema Dk. Magufuli.
Rais Dk. Magufuli leo Februari 25, 2021 anaendelea na ziara yake ya siku tatu mkoani Dar es Salaam na na shughuli zingine anazofanya leo ni kuzindua soko la Kisutu Jijini Dar es Salaam kisha atahutubia wananchi katika viwanja vya Mnazi Mmoja.